Tuesday, November 29, 2011

HIVI LINI WATANZANIA TUTABADILIKA KWA HILI SWALA LA KUCHUKUA SHERIA MKONONI?

 Mzee anaekadiliwa kua na umri wa miaka 60 walivamiwa na wananchi wenye hasira nyumbani mkoani mbeya na kuanza kumshushia kipigo cha paka mwizi,kwa kile kilichodhaniwa kumshuku ni mshirikina.
Hapa mzee wa watu akijitahidi kuomba msaada baada ya wananchi kutosikia la mtu na kumshushia kipigo.Kiukweli inasikitisha kwa haya majukumu wanayojipa wananchi maana inawezekana hata hafanyi hayo mambo na mkamsababishia mwanadam mwenzenu umauti na sijui mtasema nini kesho kwa mungu kwa kuingilia kazi yake.

DUNIA DARAJA-TWANGA PEPETA 2011

BAADA YA BABU MWAISAPILE KUWANYWESHA WATU KIKOMBE FAIDA NDIO HII

                                          Kutoka nyumba ya udongo mpaka ya kisasa.
                                      Babu akiwa katika moja ya magari yake
 Babu Mwaisapile akiwa amepumzika nyumbani kwake baada ya kazi ndefu yakuwanywesha kikombe.Hapo pembeni unaona bafu lake ni lakisasa kabisa.
Hata umeme ukikatika babu yeye kichwa hakimgongi ana solarpower,hata tanesco hataki mkataba nao.

Friday, November 18, 2011

JEMBE LANGU LINAPOKUA KAZINI KUTETEA TAIFA

Mchezaji anaecheza soka la kulipwa nchini sweden Machupa hapa akijaribu kuwatoka mabeki wa Chad katika mechi yakusaka tiketi yakucheza kombe la dunia.Mechi ilikua ya marudiano ambayo ilichezwa uwanja wa taifa na Tanzania ikitoka uwanjani kwa kudungwa goli moja kwa bila,ila Tanzania wamekwenda hatua ya makundi kwa ushindi goli la ugenini walioupata mechi ya kwanza nchini Chad.Starz walishinda 2-1.

MWANA FA FT LINAH-YALAITI

SALAMA JABIR AANZA VYEMA NA KIPINDI CHAKE KIMPYA CHA MKASI.USO KWA USO NA IRENE UWOYA

MASOUD WA KIPANYA AJA NA UPUUZI WAKE NDANI YA DVD

UPUUZI WA MASOUD KIPANYA ni documentary ya dakika 47 ambayo nimeirekodi mwaka juzi katika mazingira ya kijiji kilichotumika kurekodia MAISHA PLUS.

Mfumo nilioutumia ni kuongelea mambo mengi mchanganyiko na ili kuondoa uchovu wa kunitazama nikiongea, nimechanganya footages za videos, illustrations na animation (katuni) kuchagiza yale ninayokuwa nayazungumzia.

Ujumbe wa dvd hii ni nadharia ya vipande 26 vya keki. nikatengeneza MFANO wa uwepo wa idadi hiyo ya vipande vya keki ambavyo mara baada ya kuwekwa mbele ya watu (watanzania), kundi hilo la watu likataka kutoana roho ili kila mmmoja apate kipande cha keki hiyo, bahati nzuri wakatokea werevu (viongozi) ambao waling’amua kuwa kumbe idadi ya vipande vya keki (26) ni sawa kabisa na idadi ya watu waliokuwepo ambao walikuwa wanakaribia kutoana roho.

Werevu hawa wakawaambia watu hawa kuwa hatuna haja ya kung’oana meno wakati idadi yetu ni sawa kabisa na vipande vilivyopo, ukatengenezwa uataratibu wa kupanga foleni ili kila mmoja apite mbele achukue KIPANDE chake. baada ya kukubaliana hilo, bado werevu wakaona ni vema foleni hii iangalie walio dhaifu ili wawe mbele wawahi kupata keki kuchelea kuanguka kwa njaa.

Wakati vipande hivi vya keki vilipoanza kugawiwa, hawa viongozi, (watatu) wakaamua nao kwa kuwa ni sehem ya watu 26 kuchukua VIPANDE VYAO MAPEMA, bahati mbaya baadhi yao kutokana na kuwa karibu na meza ya keki na kutokana na ULAFI, wakaamua kuchukua zaidi ya kipande kimoja cha keki hali iliyopelekea watu wa mwishoni katika foleni ile kukosa vipande vyao.

dvd hii pia imeingia ndani kwa mafumbo kiasi kuangalia sababu inayopelekea watu kutaka kujipendelea zaidi kiasi cha kupelekea kudhulumu wengine, ikajaribu pia kuangalia dawa inayoweza kutumiwa kuepuka hali hii ya uchu na tamaa inayosababishwa na hofu ya kujiuliza nitapata lini na woga wa kuhofia kupoteza kidogo alicho nacho mkononi.

Kwanini umeitwa upuuzi? kwa sababu ya tabia na hulka za binaadam kupenda kupuuza kila kitu, ni hili nalo limetengenezwa ili ulitazame kisha ulipuuze.

Concept:
Ni documentary yenye sauti na picha za video pamoja na katuni mnato na katuni mtembeo (still cartoons and animation)

Wahusika wakuu: Masoud Kipanya

Itaingia lini sokoni: imeingia sokoni jumanne tarehe 15-11-2011 na inasambazwa na UMOJA AUDIO VISUAL.

Bei: Shilingi 3,000 tu.

Running time: Dakika 47

Sponsors: Hakuna mdhamini.

Future plans: Ni matayarisho ya upuuzi mwingine “WENYE NGUVU NA WAPAGAZI”
Nashukuru kwa ushirikiano wenu na mungu awabariki sana.

MASOUD KIPANYA.

Wednesday, November 16, 2011

HII NI MOJA YA SIRI YA JUMA NATURE KUPENDWA,POPOTE AKIKUKUTA ANAKUPA MISTARI AJALI WEWE UNA PESA WALA MASKINI.BIG UP MTOTO WA KIUMENI MWENZANGU

SHEREHE ZA MIAKA KUMI TIP TOP,KALI KULIKO ZOTE SUMA LEE AVUA VIATU NA KUMPA SHABIKI WAKE PAMOJA NA PESA ELFU 50






 Hapa Suma Lee amevua viatu na anampa pesa shabiki yake kwa saport aliompa,safi sana sio kila siku wanafanya akina 50 cent tu.

                                   Big Dady Prof Jay akiwapa mashabiki burudani
                                   Baba Wema Sepetu........D platinum

Picha zaidi tembelea kajunason.

Tuesday, November 8, 2011

MAFUTA YA TRANSFOMA YAFUPISHA MAISHA YA KIJANA HUYU.

 Kijana huyu ambae inasemekana alikua katika harakati za kuiba mafuta ya transfoma katika nguzo za umeme,Kwa taarifa ambayo imepatikana bugando jijini mwanza kila jana huyu alikutwa asubuhi ananing´inia ktk nyaya za umeme.
 Hapa mafuti wa tanesco wakiwa katika harakati za kuutoa mwili wa kijana huyo ambao uliganda katika nyaya za umeme.
                                              Hapa kijana akiwa ameshafariki
Tanesco wamelizungumzia hili kua ni tatizo kubwa sana ktk nchi ya Tanzania watu ufungua matransfoma na kuiba mafuta.
  Asante unigue entertainment.

Monday, November 7, 2011

VENGU WA ORIJINO KOMEDI HOI KITANDANI

Raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete alipotembelea hospital ya Muhimbili kuwajulia hali wagomjwa hapa akimjulia hali Vengu wa Orijino Komedi.

KWA MWENENDO HUU WANAWEZA KUSABABISHIANA KUA VIZIWI


Mambo yanazidi kuwa mambo! Kwa mara nyingine Naseeb Abdul Jumaa ‘Diamond’ anatengeneza kichwa cha habari baada ya kumbonda mwandani wake, Wema Isaac Sepetu, ni Risasi Jumamosi pekee lililosheheni habari.

NI WIVU WA KIMAPENZI
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho kazi yake ni kufuatilia mambo ya watu, Diamond anayetisha kwa sasa katika Bongo Fleva alifikia hatua ya kumtandika hadi akamharibu uso kisa kikielezwa ni wivu wa kimapenzi.
Ilidaiwa kuwa Diamond alikuta meseji ‘sms’ ya kimapenzi kwenye kilongalonga cha kiganjani cha Wema ndipo akapandwa na hasira akampa ‘kitu kinauma’.

ISHU ILIKUWA HIVI
“Ishu iko hivi; Diamond na Wema walikuwa wamepumzika mchana, ghafla jamaa alichukua simu ya Wema na kuanza kusoma sms, ndipo alipokutana na moja iliyoshiba mapenzi kutoka kwa mwanaume ikionesha kama wana uhusiano toka zamani,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
“Diamond hakutaka kuhoji zaidi, kilichofuata ni kipigo ambacho Wema hawezi kukisahau.”

WEMA KAMA MATUMLA
Chanzo kiliendelea kutambaa na mistari kuwa ilitokea purukushani kubwa ambapo Wema aligeuka bondia Mbwana Matumla kwa kupangua makonde ya Francis Miyeyusho kama alivyofanya wiki iliyopita pale Diamond Jubilee, Dar es Salaam.

DIAMOND KAMA MIYEYUSHO
Ilidaiwa kuwa staa huyo wa filamu hakufua dafu kwani Diamond alipeleka konde moja matata kama lile la Miyeyusho kwa Matumla hivyo kumwachia michoro ya makofi usoni huku akimsababishia mrembo huyo kutosikia vizuri hadi sasa.
Baada ya kuinyaka habari hiyo ikiwa ya motomoto, ‘polisi’ wa Risasi Jumamosi
alisaga soli hadi kwenye saluni ya Joan iliyopo Kijitonyama, Dar ambapo Wema alikuwa akiweka kope.

WEMA AMWAGIWA UPUPU
Baada ya kumuona paparazi wetu, Wema alihoji kulikoni ambapo alimwagiwa ‘upupu’ wote na kupewa nafasi ya kufunguka juu ya ishu hiyo.
Kwanza alianza kwa kusita, lakini baadaye alifunguka: “Jamani mapenzi nyie acheni tu, ni kweli alinipa ‘mbata’, lakini hayo ni mambo ya kimapenzi tu kwa sababu mimi mwenyewe nasikia raha sana nikipigwa na mpenzi wangu.

‘AMENITHIBITISHIA ANANIPENDA’
“Asikwambie mtu, bila kunipiga atakuwa hana wivu na mimi, lakini alivyonipiga amethibitisha anavyonipenda.
”Napenda Diamond na nitampenda maisha, kama ni vipigo sijali acheni nitoke manundu.”

WE DIAMOND, NI KWELI UMEMPIGA WEMA?
Jitihada za kumpata Diamond ili kupata jibu kama kweli alimpiga hazikuzaa matunda.

Kwa hisani ya globalpublishers.

MHH HII STYLE YA ULISHANAJI KEKI SIKU HIZI WADADA!



Thursday, November 3, 2011

BREAKING NEEEEEWS MIMI NA MSHKAJI KWA SASA PAMOJA TUNAWAKILISHA AMANI NA UPENDO

 Kiukweli katika jambo ambalo najihisi shujaa mbele ya mungu ni hili tukio nililolifanya siku ya juma3 kwa kukutana na ndugu yangu Abdallah a.k.a Dullah kumaliza tofauti zetu zilizodumu muda mrefu kama sikosei miaka 5,kiukweli namshukuru mungu mshkaji mwelevu alinielewa mara moja.Kwanza tumetoka sehem moja kiumeni pili maskani moja tatu kaka yake na baba yangu walianza safari za kutafuta maisha pamoja nje ya Tanzania miaka ya 80.

Wadau wangu nitawaomba radhi  kwa namna moja au nyingine kama nimewakwanza kuweka taarifa hii lakini kwangu nimeona ni hatua kubwa nilioifanya ndio maana nikaona nitundike.Kiufupi sina haja yakueleza tatizo lililopelekea kukosana na ndugu yangu huyu miaka 5 iliopita nafanya hivi sababu inaweza kua nimemkwanza mtu mmoja au mwingine na mimi sio lengo langu kumkwaza mtu kupitia blog yangu.

MWENYE NDOTO YAKUMFIKIA FLAVIANA MATATA HUYU HAPA JACKLINE ROBERT