Monday, January 9, 2012

DIAMOND NA MCHEZA SHOO WAKE WANUSULIKA KWENDA JELA MIEZI 6

MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul Jumaa ‘Diamond’  na wenzake wamekubali kosa la kumshambulia mwandishi Francis Godwin na kuhukumiwa kwenda jela miezi sita kila mmoja ama kulipa faini ya shilingi elfu hamsini (50,000/=) kwa kila mmoja ikiwa ni pamoja na kulipa shilingi elfu thelathini (30,000/=) kwa Godwin.

Watuhumiwa wamelipa faini hiyo japo mwanahabari huyo hajapokea fedha hiyo na anakusudia kukata rufaa katika mahakama ya juu zaidi. Chanzo: