Sunday, August 14, 2011

KAKA ABRAHAM ALIPOTUKUTANISHA KATIKA FTARI YA PAMOJA JANA.

 Asante kaka Abraham kwa mungu kukupa moyo na kutukutanisha pamoja maana ni lazma mungu akutunuku kila mtu anatamani kufanya hivi ila mungu ndio anaeweza kumpa mtu ujasili na maamuzi kama haya Inshallah upate malipo mema leo na kesho kiama kwa barka za ramadhani amen.

 Kaka Naaman alijumuika katika ftari.


 Kaka Khamis na Twarib wakijipendelea




 Shekh Yunus hakua nyuma kabisa na jana wote kwa pamoja tulimchagua kua muweka hazina wa mfuko wa sikukuu ya eid tulifanya hivyo sababu anauzoefu na hiyo nafasi.
 Mwamba mdogo
 Mchezaji wa Barca ya moro nae alikuwepo.

 Mrisho
                                 Mjomba JJ na Liban wakichukua chao mapema.
                                 Mwamba mwenyewe

 Wadau msishangae ujazo wa sahani yangu na hapo nilirudi mezani mara mbili tena.Kiukweli mimi na kula tunapendana sana na mapenzi yetu na chakula hayatoisha na ukizingatia jana swaum ilinishika sana niliipania ftari.

 Kaka Said nae akiwajibika katika ftari
 Kaka Mweneu  huyu jamaa ndio aliopatwa na mtihani wa kufiwa na mdogo wake South africa na tulijaaliwa kumfanyia dua baada ya ftari.
 Upande wa kina mama na watoto nao wakipata Ftari safi sana wazazi kwa kuongoza vyema katika msimamo wa dini huku ugenini najua si kazi ndogo ila mimi nawaombea mungu awaongezee ujasili wa kuwasimamia vijana wetu katika kufata maadili ya kidini.Amen

 Dada na mdogo wake
 kua mtulivu wakati wa kula ukimaliza unaweza kuongea hata dini yetu inatuambia hivyo.

 Sachimoo na Khamis wakiteta huku ftari inaendelea
 Muongozo wetu huu wa hapa Stockholm Shekh juma nae aliudhulia
 Watu wa London nao walipanda ndege kuitikia wito wa ftari Stockholm sasa mimi ninaepanda bus kwanini nishindwe kwenda kumpa thawabu alietuandalia ftari.Hapa wakishow love baada ya ftari

Wandugu wakipata picha ya pamoja baada ya ftari na ndio walikua wapishi wakuu wa ftari yetu jana mungu atawalipa kwa kujitolea kwa ajili yake amen.